Thursday 3 September 2009

Arsenal kumkatia rufaa Eduardo
Arsenal imethibitisha kuwa imepokea rasmi taarifa ya UEFA ya kumfungia Mchezaji wao kutoka Croatia, Eduardo, baada ya kupatikana na hatia ya kumdanganya Refa kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Celtic na kupata penalti aliyofunga bao la kwanza katika ushindi wa 3-1 na baada ya kuichambua wameamua kukata rufaa kuipinga adhabu hiyo.
Taarifa ya Arsenal iliyochapishwa kwenye tovuti yao ilisema kuwa Klabu baada ya kupokea taarifa ya UEFA kuhusu adhabu ya Eduardo wanaamini ina kasoro na haina misingi ya ushahidi thabiti kwa hiyo wameamua kukata rufaa.

No comments:

Powered By Blogger