Thursday 3 September 2009

MWANA WA FERGUSON APIGWA FAINI NA KUFUNGIWA!!!
Meneja wa Peterborough, Darren Ferguson, ambae ni mtoto wa Sir Alex Ferguson wa Manchester United, amepatikana na hatia ya kutoa lugha chafu kwa Refa mara baada ya Timu yake kufungwa 3-2 na West Brom kwenye mechi ya Ligi ya Daraja liitwalo Championship ambalo ni chini tu ya Ligi Kuu.
Darren Ferguson amepigwa faini ya Pauni 750 na kufungiwa mechi 2 kutokaa benchi la akiba lakini adhabu ya kufungiwa mechi 2 imesimamishwa ili kuchunguza mwenendo wake na itatumika tu akifanya kosa lolote msimu huu.

No comments:

Powered By Blogger