Monday 31 May 2010

Nigeria yataja 23 wa Bondeni!
Kocha wa Nigeria, Lars Lagerback, amewatupa nje Ikechukwu Uche wa Real Zaragoza na Straika wa Everton, Victor Anichebe, na kutangaza Kikosi chake cha mwisho cha Wachezaji 23 watakaokwenda Afrika Kusini katika Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 11.
Katika Kikosi hicho yupo ‘majeruhi’ John Mikel Obi wa Chelsea ambae alikuwa akiuguza goti lake baada ya kufanyiwa operesheni.
Nigeria wapo Kundi B pamoja na Argentina, Ugiriki na Korea Kusini.
Mechi yao ya kwanza ni Juni 12 dhidi ya Argentina.
Kikosi kamili ni:
MAKIPA: Vincent Enyeama (Hapoel Tel Aviv, Israel), Dele Aiyenugba (Bnei Yehuda, Israel), Austin Ejide (Hapoel Petah Tikva, Israel)
MABEKI: Taye Taiwo (Marseille, France), Elderson Echiejile (Rennes, France), Chidi Odiah (CSKA Moscow, Russia), Joseph Yobo (Everton, England), Daniel Shittu (Bolton Wanderers, England), Ayodele Adeleye (Sparta Rotterdam, Netherlands), Rabiu Afolabi (SV Salzburg, Austria)
VIUNGO: Chinedu Ogbuke Obasi (TSG Hoffenheim, Germany), John Utaka (Portsmouth, England), Kalu Uche (Almeria, Spain), Dickson Etuhu (Fulham, England), John Mikel Obi (Chelsea, England), Sani Kaita (Alaniya, Russia), Haruna Lukman (AS Monaco, France), Yusuf Ayila (Dynamo Kiev, Ukraine), Osaze Odemwingie (Lokomotiv Moscow, Russia)
MASTRAIKA: Yakubu Aiyegbeni (Everton, England), Nwankwo Kanu (Portsmouth, England), Obafemi Martins (Wolfsburg, Germany), Victor Obinna Nsofor (Malaga, Spain)

No comments:

Powered By Blogger