Wednesday 2 June 2010

Zimbabwe 0 Brazil 3
Leo huko Harare, Zimbabwe, Uwanja wa Taifa, Brazil ambayo ipo Afrika Kusini kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia, imeichapa Zimbabwe bao 3-0 katika mechi ya kirafiki.
Hadi mapumziko, Brazil ilikuwa mbele kwa bao 2-0 wafungaji wakiwa Bastos dakika ya 42 na Robinho dakika ya 44.
Elano aliongeza bao la 3 kwenye dakika ya 56.
Brazil watasafiri kwenda Dar es Salaam, Tanzania kucheza na Taifa Stars, Timu ya Taifa ya Tanzania, hapo Jumatatu Juni 7.
Brazil wapo Kundi G kwenye Fainali za Kombe la Dunia pamoja na Korea Kaskazini, Ivory Coast na Ureno.
Brazil watacheza mechi yao ya kwanza Juni 15 dhidi ya Korea Kaskazini.

No comments:

Powered By Blogger