Tuesday 1 June 2010

Kikosi cha ENGLAND Kombe la Dunia chatajwa!!!
• Leighton Baines, Michael Dawson, Tom Huddlestone, Scott Parker, Adam Johnson, Theo Walcott & Darren Bent NJE!!!!.
Hatimaye Fabio Capello ametangaza Kikosi chake cha Wachezaji 23 ambao atasafiri nao hapo kesho kwenda Afrika Kusini tayari kwa Fainali za Kombe la Dunia linaloanza Juni 11.
Majina hayo ya Wachezaji 23 yanatakiwa yafikishwe FIFA leo.
Wachezaji waliotolewa na kuachwa toka Kikosi cha awali cha Wachezaji 30 ni Leighton Baines, Michael Dawson, Tom Huddlestone, Scott Parker, Adam Johnson, Theo Walcott na Darren Bent.
Miongoni mwa Wachezaji hao 23 ni Kiungo wa Manchester City, Gareth Barry, ambae bado anauguza enka lakini amechukuliwa kwa mategemeo atapona.
Kikosi hicho kinaongozwa na Nahodha Rio Ferdinand.
England wapo Kundi C pamoja na USA, Algeria na Slovenia na watacheza mechi yao ya kwanza Juni 12 dhidi ya USA.
Kikosi kamili:
MAKIPA: Joe Hart, David James, Robert Green.
MABEKI: Jamie Carragher, Ashley Cole, Rio Ferdinand, Glen Johnson, Ledley King, John Terry, Matthew Upson, Stephen Warnock
VIUNGO: Gareth Barry, Michael Carrick, Joe Cole, Steven Gerrard, Frank Lampard, Aaron Lennon, James Milner, Shaun Wright-Phillips.
MAFOWADI: Peter Crouch, Jermain Defoe, Emile Heskey, Wayne Rooney

No comments:

Powered By Blogger