
Kocha wa Korea Kaskazini, Kim Jong-hun, alitangaza Majina ya Makipa wawili tu na kumtaja Straika Kim kuwa ni Kipa wa Tatu.
Korea Kaskazini wako Kundi G pamoja na Brazil, Ivory Coast na Ureno.
FIFA imetoa stetimenti kuelezea hali hiyo ya Korea Kaskazini na imesema: “Listi za Wachezaji 32 kwa kila Timu zilizowasilishwa kwetu Juni 1 ni za mwisho na haziwezi kubadilishwa. Listi hiyo ya Wachezaji 32 inataka Makipa wawe watatu. Kitu pekee kinachoweza kubadili listi hizo ni endapo Mchezaji ataumia vibaya Masaa 24 kabla ya Mechi ya kwanza, Mchezaji huyo anaweza kubadilishwa. Wachezaji watatu waliotajwa kama Makipa wanaruhusiwa kucheza nafasi ya Kipa tu kwenye Fainali hizi za Kombe la Dunia na hili limetangazwa kwa kila Timu. Hivyo Kim Myong-won haruhusiwi kucheza kama Straika.”
No comments:
Post a Comment