Monday 15 September 2008



CHELSEA WAIKATIA RUFAA KADI NYEKUNDU YA NAHODHA JOHN TERRY!!

Klabu ya Chelsea leo imekata rufaa kwa FA kupinga kadi nyekundu aliyopewa Nahodha wao John Terry juzi kwenye mechi na Manchester City iliyochezwa Uwanja wa City of Manchester ambayo Chelsea walishinda 3-1.
Kwa mujibu wa ripoti ya Refa Mark Halsey, John Terry alipewa kadi nyekundu kwa kucheza rafu mbaya na si kwa kumzuia Mshambuliaji wakati akiwa ndio beki wa mwisho ambayo kitaaluma huitwa 'rafu ya kiprofesheni'.
Rufaa hii itasikilizwa kesho.
Endapo rufaa itabwagwa basi Nahodha John Terry atakosa mechi tatu ya kwanza ya Jumapili tarehe 21 Septemba 2008 zidi ya Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United, ya pili ni ya Kombe la Carling watakayocheza na Portsmouth Septemba 24 na ya mwisho na Stoke City ambalo ni pambano la LIGI KUU.

No comments:

Powered By Blogger