Wednesday 17 June 2009

BONDENI 2 NEW ZEALAND 0
NEW ZEALAND NJE MABARA!!
Bao mbili zilizopigwa na Parker zimewang’oa New Zealand nje ya Kombe la Mabara na kuwapa matumaini Wenyeji Afrika Kusini kuingia Nusu Fainali ya Kombe hili.
Ili kujihakikishia kuingia Nusu Fainali Afrika Kusini wanahitaji suluhu na Spain ambao wameshatinga Nusu Fainali na matokeo hayo ni ya bila kujali mechi kati ya Iraq na New Zealand.
Endapo Iraq akifungwa au akitoka sare kwenye mechi hiyo, Afrika Kusini atatinga Nusu Fainali.
VIKOSI:
AFRIKA KUSINI: Khune, Gxa, Masilela, Mokoena, Sibaya, Pienaar, Modise, Dikgacoi, Booth, Prker
NEW ZEALAND: Moss, Locchead, Vicelich, Elliot, Brown, Smeltz, Killen, Bertos, Christie, Mulligan, Boyens
Korea Kaskazini ndani ya FAINALI KOMBE LA DUNIA 2010!!!
Kwa mara ya kwanza tangu 1966 walipoushangaza ulimwengu walipocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Uingereza na kutinga Robo Fainali na kuongoza 3-0 hadi mapumziko ingawa kwenye mechi hiyo walikung’utwa 5-3 na Ureno ya Eusebio wakati huo, leo Korea Kaskazini wametinga tena Fainali za Kombe la Dunia Afrika Kusini mwaka 2010 baada ya kutoka suluhu 0-0 na Saudi Arabia.
Mafanikio ya Korea Kaskazini pia yamesaidiwa na Iran kushindwa kuifunga Korea Kusini huko Seoul, mji mkuu wa Korea Kusini.
Sasa Korea Kaskazini wanaungana na wenzao Korea Kusini, Japan na Australia kutoka KUNDI la Nchi za Asia, pamoja na Uholanzi kutoka Ulaya, kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwaka 2010.
Saudi Arabia bado wana nafasi ya kuingia Fainali za Kombe la Dunia kwani Septemba watacheza mechi na jirani zao Bahrain na mshindi atakumbana na New Zealand ili kupata Nchi moja itakayoingia Fainali.

No comments:

Powered By Blogger