Wednesday 17 June 2009

DROGBA AFUNGIWA MECHI 6, BOSINGWA 4 NA CHELSEA FAINI PAUNI ELFU 85!!!!
UEFA leo imemdunga Didier Drogba kifungo cha mechi 6 na mwenzie Jose Bosingwa mechi 4 kufuatia kasheshe waliyoileta baada ya mechi ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE Uwanjani kwao Stamford Bridge Chelsea walipotolewa na Barcelona kwa goli la ugenini.
Katika mechi hiyo iliyochezwa Mei 6 na kuchezeshwa na Refa Tom Henning Ovrebo kutoka Norway na kumalizika 1-1 na Chelsea kuminywa si chini ya penalti 3 au 4 za wazi, Drogba alimvaa Refa mara baada ya filimbi ya mwisho na kumtukana huku Walinzi wakimzuia kwa nguvu asimkaribie Refa huyo.
Nae Jose Bosingwa alikaririwa baada ya mechi akimwita Refa ni ‘mwizi'.
Drogba atazikosa mechi 4 tu za Mashindano ya UEFA msimu ujao na mechi 2 zitasimamishwa kwa miaka miwili ili kuchunguza mwenendo wake.

Bosingwa atakosa mechi 3 huku ya 4 ikisimamishwa kwa miaka miwili ili kuchunguza mwenendo wake.
Mbali ya adhabu hiyo kwa Wachezaji hao wawili wa Chelsea, Klabu yenyewe imetwangwa faini ya Pauni Elfu 85 kwa kushindwa kuwadhibiti Wachezaji na Washabiki wao waliotupa vitu Uwanjani baada ya mechi
Drogba, Bosingwa na Klabu yao wamepewa siku 3 ili kukata rufaa..

No comments:

Powered By Blogger