Saturday 20 June 2009

TEVEZ KUONDOKA MAN U!!!
Mabingwa wa England, Manchester United, wametoa taarifa kupitia tovuti yao kuwa Carlos Tevez hataendelea kuwepo hapo Klabuni baada ya Washauri wake kuwajulisha kuwa wamekataa ofa ya Man U ya mkataba wa miaka mitano, ada ya Pauni Milioni 25.5 na pia kumfanya awe mmoja wa Wachezaji wenye mshahara mnono sana hapo klabuni.
Taarifa ya Man U ilisema: ‘Kufuatia taarifa tulizopokea jana usiku kutoka kwa Washauri wa Carlos Tevez ikiwa ni mbele ya siku ya mwisho Klabu iliyoweka ili makubaliano yafikiwe, Manchester United inatangaza kuwa Carlos Tevez hatasaini mkataba mpya na Klabu yetu.’
‘Klabu ilikubali kulipa Pauni Milioni 25.5, kumpa mkataba wa miaka mitano na mshahara mkubwa wa kumfanya awe ni miongoni mwa Wachezaji wanaolipwa juu. Lakini, kwa masikitiko, Washauri wake wametujulisha, ingawa alipata mafanikio makubwa sana hapa Klabuni, hataki kuendelea kucheza hapa.
‘Klabu inapenda kumshukuru Carlos kwa utumishi wake kwa misimu miwili iliyopita na inamtakia kila la heri maisha yake ya baadae’
Tevez alichukuliwa na Man U kutoka West Ham kwa mkopo kutoka Kampuni inayommiliki kwa mkataba wa miaka miwili unaokwisha Juni 30.

No comments:

Powered By Blogger