Thursday 18 June 2009

Huko Bondeni VUVUZELA laleta kasheshe!!!
FIFA kulijadili!!!!
Makampuni makubwa ya TV kutoka Ulaya yanayorusha matangazo ya moja kwa moja ya mechi za Kombe la Mabara huko Afrika Kusini yamepeleka malamiko yao kwa FIFA wakikerwa na ‘VUVUZELA’.
VUVUZELA ni tarumbeta la plastiki ambalo hutumiwa na Mashabiki wa Bondeni kushangilia Timu zao zinapocheza na hupulizwa mfululizo kwenye mechi.
VUVUZELA ni desturi na ndio utamaduni wa Mashabiki wa Bondeni.
Lakini, Makampuni ya TV yamekerwa na sasa FIFA watafanya kikao kulijadili VUVUZELA.

Lakini, Mashabiki wa Bondeni wamesema VUVUZELA litadumu!!!

No comments:

Powered By Blogger