Saturday 20 June 2009

Man City wamtwaa Santa Cruz
Manchester City wamefikia makubaliano na Blackburn Rovers ya kumnunua Straika kutoka Paraguay Roque Santa Cruz, 27, kwa ada ya Pauni Milioni 18.
Ununuzi wa Santa Cruz umekuwa wa taabu kwa vile kuna kipengele kwenye mkataba wake kwamba anaetaka kumnunua lazima ailipe Blackburn Pauni Milioni 18 juu ya ada ya uhamisho kwa vile mkataba wake unamalizika 2012.
Santa Cruz, alinunuliwa na Blackburn kutoka Bayern Munich mwaka 2007 kwa Pauni Milioni 3.8, ameichezea Blackburn mechi 70 na kufunga mabao 29. Msimu huu amekuwa akicheza kwa nadra sana kwa kusumbuliwa na goti.
Dili hii ya Santa Cruz ikikamilika huyu atakuwa Mchezaji wa pili kununuliwa na Man City baada ya kumnunua Gareth Barry kutoka Aston Villa.
Santa Cruz hapo Man City ataungana tena na Meneja Mark Hughes, mtu aliemnunua kutoka Bayern Munich alipokuwa Meneja wa Blackburn
Chelsea yakata rufaa UEFA kupinga adhabu za Drogba, Bosingwa!!!!!
Chelsea wamethibitisha kuwa wamekata rufaa UEFA kupinga ukali wa adhabu za Didier Drogba na Jose Bosingwa zilizotelewa na UEFA kufuatia kasheshe la kumkashifu Refa Tom Henning Ovrebo mara baada ya mechi ya NUSU FAINALI ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE ambayo Andres Iniesta aliisawazishia Barcelona dakika za majeruhi na kuwaingiza Barcelona Fainali kwa goli la ugenini.
Drogba amefungiwa mechi 6, mechi mbili zikisimamishwa kwa miaka miwili kuchunguza mwenedo wake, na Bosingwa, aliemwita Refa huyo kutoka Norway ‘mwizi’, amefungiwa mechi 4 huku moja ikiwekwa kiporo kuchunguza mwenendo wake.
Vilevile Chelsea imesema itakata rufaa kupinga Klabu kupigwa faini ya Pauni 85,000 kwa kushindwa kuwadhibiti Wachezaji pamoja na Mashabiki yake waliokuwa wakirusha ‘makombora’ uwanjani baada ya mechi kwisha.
Wigan wamsaini Gomez kutoka Espanyol
Meneja mpya wa Wigan Roberto Martinez amefanya usajili wake wa kwanza kwa kumchukua Kiungo Jordi Gomez kutoka Espanyol ya Spain kwa mkataba wa miaka mitatu na ada yake ya uhamisho imekadiriwa kuwa ni Pauni Milioni 1.7.
Meneja Martinez alikuwa na Mchezaji huyo huko Swansea msimu uliokwisha ambako Gomez alikuwa akicheza kwa mkopo na Martinez akiwa ndie Meneja wa Swansea.

Gomez, 24, aliifungia Swansea mabao 14.

No comments:

Powered By Blogger