Thursday 18 June 2009

Brazil yanusa Nusu Fainali, waichapa USA 3-0!!!
Mabingwa wa Marekani ya Kusini, ambao pia ndio Watetezi wa Kombe la Mabara, Brazil, wanainusa Nusu Fainali ya Kombe la Mabara, baada ya kuifunga USA mabao 3-0 katika mechi ya KUNDI B iliyochezwa leo huko Tshwane, Pretoria Uwanja wa Loftus Versfeld.

Ikiwa Misri watafungwa na Mabingwa wa Dunia Italia, Brazil watajihakikishia Nusu Fainali.
Mabao ya Brazil yalifungwa na Felipe Melo, dakika ya 7, Robinho, dakika ya 20, na Maicon, dakika ya 62.
Katika mechi ya kwanza Brazil waliwafunga Mabingwa wa Afrika, Misri, 4-3.
VIKOSI:
Brazil: Julio Cesar, Maicon, Lucio, Felipe Melo, Gilberto Silva, Luis Fabiano, Kaka, Robinho, Miranda, A. Santos, Ramires.
USA: Howard, Bornstein, Onyewu, Beasley, Dempsey, Donovan, Bradley, Demert, Kljestan, Altidore, Spector
REFA: Massimo Bussaca [Switzerland[
RATIBA: LEO SAA 3 NA NUSU USIKU [BONGO TAIMU] MISRI v ITALY
Bayern yamnyemelea Bosingwa!!!!
Bayern Munich imekubali kuwa inamtaka Beki kutoka Ureno wa Chelsea, Jose Bosingwa, ingawa mpaka sasa Klabu hizo mbili hazijafikia makubaliano.
Mwenyekiti wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummnigge amesema: ‘Tupo mazungumzoni, tunahitaji Chelsea wakubali.’
Bayern Munich wana pengo la Beki wa kulia baada ya Willy Sagnol kulazimika kustaafu na Massimo Oddo, alie Bayern kwa mkopo kutoka AC Milan,kuwa chini ya kiwango.
Sir Bobby Charlton asema ada ya Ronaldo ni ‘mbaya’ lakini sahihi!!!!
Mkongwe wa Manchester United ambae sasa ni mmoja wa Wakurugenzi wa Klabu hiyo, Sir Bobby Charlton, amesema Manchester United walikuwa na kila haki kudai ada ambayo ni rekodi ya dunia kwa Mchezaji Bora Duniani.
Ingawa amekiri ada hiyo ni ‘uchafu’, amesema ni haki ya Klabu yake kuidai. Ronaldo ameuzwa kwa Real Madrid kwa Pauni Milioni 80 na ada hiyo imezua mijadala mingi na mirefu.
Charlton anasema: ‘Dili ni nzuri na ya haki! N pesa nyingi, ni wehu! Lakini kama Kampuni na kama Klabu tuna majukumu yetu. Ronaldo anatutoka kwa sababu ni ndoto yake kwenda Real Madrid. Tumembariki aondoke!’
Santa Cruz asikitishwa hakuna Klabu inayomtaka!!!

Mshambuliaji kutoka Paraguay, Roque Santa Cruz, ameanza kukata tamaa kuwa hakuna Klabu itakayoweza kumnunua kutoka Klabu yake ya sasa Blackburn Rovers kwa sababu mkataba wake una kipengele kigumu kinachotaka Klabu kuilipa Blackburn Pauni Milioni 20 juu ya ada ya kawaida ya uhamisho kwa sababu hajamaliza mkataba wake unaoisha 2012.
Manchester City walimuwania Januari lakini wakagonga mwamba kutokana na kipengele hicho.

No comments:

Powered By Blogger