Thursday 18 June 2009

Mabingwa wa Dunia chali kwa Misri!!
Mabingwa wa Dunia Italia wamepigwa kimoja na Mabingwa wa Afrika Misri na sasa ni hekaheka nani ataingia Nusu Fainali kwenye KUNDI lao.
KUNDI B Brazil ndio vinara wana pointi 6, Italia pointi 3 na Misri pointi 3.
Mechi za mwisho ni Brazil v Italia,na huu ni moto kwa Italia kwani lazima washinde, Misri wanacheza na USA ambao, kwa hesabu za juu juu, washaaga Mashindano haya ingawa wana nafasi finyu ikiwa Brazil atashinda halafu wao wawatandike Misri kwa idadi bora ya magoli .

No comments:

Powered By Blogger