Tuesday 16 June 2009

MISRI WAKATA RUFAA FIFA KUHUSU MAAMUZI YA REFA WEBB!!
FIFA imepokea malamiko rasmi kutoka Misri ambayo jana katika mechi ya kwanza ya KUNDI B kugombea Kombe la Mabara huko Afrika Kusini ilipigwa bao 4-3 na Brazil huku bao la ushindi la Brazil likifungwa kwa penalti dakika za majeruhi.
Refa aliechezesha pambano hilo ni Mwingereza Howard Webb na alionekana akiashiria kuwa ipigwe kona lakini akabadili uamuzi na kumtoa Mlinzi wa Misri Ahmed El Mohamady kwa Kadi Nyekundu na kuwapa Brazil penalti iliyofungwa na Kaka.
Misri hawapingi uamuzi wa Refa Howard Webb kutoa Kadi Nyekundu na penalti ila wanachopinga ni jinsi Refa huyo alivyoutoa uamuzi huo.
Misri pia hawapingi kuwa Mchezaji wao aliushika mpira bali wanachodai ni kuwa Refa aliamua ipigwe kona kwa sababu yeye na Mshika Kibendera hawakuliona tukio lakini, wakati Mchezaji alietenda madhambi akivunga kaumia, ndipo akajulishwa na Mwamuzi wa Akiba kwa redio baada ya kuona marudio ya tukio hilo kwenye video.
Kocha Msaidizi wa Misri, Gharib Chawki, anadai: ‘Tunavyojua sheria haziruhusu matumizi ya video kwa Marefa.’
Hata Mchezaji wa Brazil, Luis Fabiano, amekiri kuwa Refa na Msaidizi wake hawakuliona tukio ila walijulishwa kwa redio na Mwamuzi wa Akiba, Matthew Breeze, kutoka Australia.
Utata huu unaikumbusha dunia lile tukio lililotokea kwenye Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2006 pale Zinedine Zidane alipotolewa kwa Kadi Nyekundu kwa kumtwanga kichwa Materazzi wa Italy katika tukio ambalo Waamuzi hawakuliona bali walijulishwa na Mwamuzi wa Akiba ambae pia hakuliona ila marudio yake kwenye video ndio aliyoyaona na kumtonya Refa kwa redio.
Hata hivyo FIFA siku zote imekuwa ikiyakataa madai hayo.

Hamna Sheria ya Soka inayotamka Refa atasaidiwa na matumizi ya video.
RATIBA KOMBE LA MABARA [saa za Bongo]
-Jumatano 17 Juni 2009-06-05
KUNDI A
Spain v Iraq [saa 11 jioni]
Afrika Kusini v New Zealand [saa 3 na nusu]
-Alhamisi 18 Juni 2009
KUNDI B
USA v Brazil [saa 11 jioni]
Egypt v Italia [saa 3 na nusu usiku]
WIGAN WAMCHUKUA MARTINEZ KUWA MENEJA!!!!
Wigan Athletic wamethibitisha kuwa Roberto Martinez [35] , kutoka Spain, ndie Meneja wao mpya atakaerithi nafasi iliyoachwa wazi na Steve Bruce aliekwenda Sunderland.
Roberto Matinez ametokea Klabu ya Daraja la Chini Swansea na amesaini mkataba wa miaka mitatu.
Wakati akiwa Mchezaji, Martinez alizichezea Klabu za Wigan na Swansea na mwaka 2007 akapewa nafasi ya Umeneja huko Swansea na akamudu kuipandisha Swansea kuingia Ligi Wani katika msimu wake wa kwanza tu.
LIVERPOOL WAMNYAKUA GLEN JOHNSON!!!
Klabu ya Liverpool imefanikiwa kumchukua Beki wa Portsmouth, Glen Johnson [24] kwa dau la Pauni milioni 17.
Klabu za Chelsea na Manchester City pia zilikuwa zikimuwania Beki huyo wa zamani wa Chelsea iliyomuuza kwenda Portsmouth mwaka 2006 kwa Pauni Milioni 4 tu lakini mwenyewe akaichagua Liverpool.
Sasa inaelekea Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, atamuuza Beki Andrea Dossena ili kupata dau la kununua Wachezaji.
DRO YA RAUNDI YA KWANZA CARLING CUP YAFANYWA!!
Ratiba ya Raundi ya kwanza ya Kombe la Carling imetolewa na kama kawaida Klabu za LIGI KUU England huwa hazishirikishwi duru hili.
Mechi za Raundi hii zitafanyika kuanzia Agosti 10.
Klabu pekee iliyoporomoka Daraja kutoka LIGI KUU na kupangwa kwenye Raundi hii ya kwanza ni West Bromwich Albion watakaokumbana na Bury.
RATIBA KAMILI NI:
Accrington Stanley v Walsall
Huddersfield v Stockport
Rotherham v Derby
Tranmere v Grimsby
Sheffield Wednesday v Rochdale
Bury v West Brom
Notts County v Doncaster
Lincoln v Barnsley
Scunthorpe v Chesterfield
Coventry v Hartlepool
Darlington v Leeds
Preston v Morecambe
Crewe v Blackpool
Carlisle v Oldham
Nottingham Forest v Bradford
Macclesfield v Leicester
Sheffield United v Port Vale
Cardiff v Dagenham & Redbridge
Wycombe v Peterborough
Southampton v Northampton
Barnet v Watford
Hereford v Charlton
Bristol Rovers v Aldershot
Millwall v Bournemouth
Gillingham v Plymouth
Colchester v Leyton Orient
Reading v Burton Albion
Exeter v Queens Park Rangers
Cheltenham Town v Southend
Brentford v Bristol City
Yeovil v Norwich City
Crystal Palace v Torquay
MK Dons v Swindon
Swansea v Brighton & Hove Albion
Shrewsbury v Ipswich
REAL MADRID KUWATEMA LUNDO LA WACHEZAJI!!!
Baada ya kutobokewa mifuko kwa kuwanunua Ronaldo na Kaka kwa bei mbaya sana, Real Madrid sasa inawabidi kuuza lundo la Wachezaji na Maafisa wake sasa wanahaha Ulaya nzima na hasa England kutafuta soko kwa Wachezaji hao.
Wachezaji ambao Real Madrid inataka kuwauza ni Arjen Robben, Van Nistelrooy, Klaas-Jan Huntelaar, Wesley Sneijder, Rafael van der Vaart, Royston Drenthe, Gabriel Heinze, Mahamadou Diarra na Javier Saviola.
Inasemekana Huntelaar na Van Nistelrooy huenda wakaenda Tottenham.
Mwenyekiti Bayern Munich asema Man U, Chelsea na Barca wametoa ofa kwa Ribery!!!
Mwenyekiti wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge, ametoboa kuwa Vilabu vya Manchester United, Chelsea na Barcelona vimetoa ofa rasmi kumnunua Kiungo wao kutoka Ufaransa Franck Ribery.
Rumenigge amesema: ‘Hatuna mchecheto! Tumewakatalia Real Madrid kumnunua Ribery! Na pia Man U, Chelsea na Barca wametoa ofa! Lakini sisi ndio wenye nguvu na hatumuuzi!’
Wadau wengi wanaamini kauli na msimamo huo wa Bayern Munich ni ule ule kama walivyowafanyia Manchester United walipotaka kumnunua Owen Hargreaves na hatimaye wakamuuza kwa bei ambayo ilikuwa juu mno.
.

No comments:

Powered By Blogger