Monday 15 June 2009

Italy 3 Marekani 1
Mechi ya pili ya KUNDI B imewakutanisha Mabingwa wa Dunia Italy na USA ndani ya Uwanja wa Loftus Versfeld, uliopo Tshwane, Pretoria.
Kipindi cha kwanza USA walipata pigo kubwa pale Clark alipoivaa Kadi Nyekundu kwenye dakika ya 33 baada ya Refa kutoka Chile, Pablo Pozo, kuamua amecheza rafu mbaya dhidi ya Gattuso.
Hata hivyo, Marekani hawakukata tamaa na waliendelea kuwabana Italy na hatimaye ilipofika dakika ya 40 Refa Pozo akawapa penalti baada ya Chiellini kucheza faulo kwa Altidore na Nahodha Landon Donovan akamhadaa vizuri Kipa Buffon wa Italy na kupachika bao kwa USA.
Mapumziko: USA 1 Italy 0
Kipindi cha pili, kwenye dakika ya 57, Kocha Marcello Lippi akafanya mabadiliko na kuwaingiza Giuseppe Rossi, bwana mdogo wa zamani Man U badala ya Mkongwe Gattuso, na Montolivi badala ya Camoranes.
Dakika moja baadae Giuseppe Rossi akapiga mkwaju wa mbali uliomshinda Tim Howard, Kipa wa USA ambae zamani walikuwa nae Man U, na mechi kuwa 1-1.
Dakika ya 72, Tim Howard tena alizidiwa na shuti la mbali liliopigwa na Daniele De Rossi ingawa ana kila sababu ya kuwalaumu Mabeki wake kwa kumchuuza.
Lakini goli la 3 la Giuseeppe Rossi, kama la kwanza, Tim Howard hawezi kulaumu mtu au kulaumiwa, ni kigongo kisichozuilika.
USA: HOWARD, BORNSTEIN, ONYEWU, DEMPSEY, DONOVAN, BRADLEY, CLARK, DEMERIT, ALTIDORE, SPECTOR, FEILHABER
ITALY: BUFFON, GROSSO, CHIELLINI, LEGROTTAGLIE, GATTUSO, DE ROSSI, GILARDINO, IAQUINTO, CAMORANES,ZAMBROTTA, PIRLO
REFA: Pablo Pozo [Chile]

No comments:

Powered By Blogger