Monday 15 June 2009

Brazil 4 Misri 3
Mabingwa wa Afrika, Misri, licha ya kufungwa imeonyesha waziwazi sasa Afrika si mdebwedo baada ya kuwabana na kutishia kuwabwaga Vigogo wa Soka Brazil na mpaka ikabidi Brazil wapate goli la ushindi kwa njia ya penalti dakika ya 90 baada ya Beki A. Elmohamadi kudaka mpira akiwa mstari wa golini na Refa Mwingereza anaechezesha Ligi Kuu, Howard Webb, akamzawadia Kadi Nyekundu na kuamuru ipigwe penalti iliyofungwa na Mchezaji mpya wa Real Madrid, Kaka.
Brazil ndio waliotangulia kupata bao kupitia Kaka dakika ya 5, lakini Mchezaji machachari wa Misri Zidan akasawazisha dakika ya 9.
Brazil wakapachika mabao mawili dakika ya 12 kupitia Luis Fabiano na Mlinzi Juan akafunga kwa kichwa dakika ya 32.
Hadi mapumziko Brazil 3 Misri 2.
Kipindi cha pili, Misri wakaweza kurudisha mabao yote ndani ya dakika moja tu pale Shawky, anaechezea Middlesbrough, kufunga bao la pili dakika ya 54 na Zidan kurudisha la 3 dakika moja baadae.
Huku wengi wakiamini ngoma droo ndipo kizaazaa kwenye goli la Misri kufuatia kona kikamfanya Beki Elmohamadi kuuzuia mpira uliokuwa unatinga wavuni kwa mkono na Refa Howard Webb wa England hakubabaika na akamtwanga Kadi Nyekundu na kuamuru ipigwe penalti aliyofunga Kaka bao la 4.
VIKOSI:
Brazil: Julio Cesar, Lucio, Juan, Felipe Melo, Kleber, Elano, Gilberto Silva, Luis Fabiano, Kaka, Robinho, Dani Alves.
AKIBA: Maicon, Victor, Luisao, Miranda, A. Santos, Ramires, Julio Baptista, Kleberson, Pato, Nilmar, Gomes, Josue.
Egypt: El Hadary, A. Said, Hani, A. Fathi, Hosni, Zidan, M. Shawky, A. Hassan, Wail gomaa, Abo Terika.
AKIBA: M. Fathalla, A. Elmohamadi, A. Khairy, A. Eid, M. Homas, A. Tawfik, A. Farag, Wahid, A. Abdelghani, Abo Grusha, A. Raouf, M. Sobhi
REFA: Howard Webb [England]

SAA 3 NA NUSU USIKU [BONGO TAIMU] NI USA v ITALY

No comments:

Powered By Blogger