Wednesday 15 July 2009

Adebayor akaribia kutua Man City
Mshambuliaji toka Togo na Arsenal, Emmanuel Adebayor, anaelekea kukaribia kuwa Mchezaji mpya wa Manchester City baada ya kufaulu vipimo vya afya na pia kupata Kibali cha Kazi.
Man City katika wiki hii moja imemnasa Carlos Tevez na Nahodha wa Chelsea, John Terry, yupo mbioni kujiunga ingawa mpaka sasa Chelsea wanang’ang’ana hauzwi.
Klabu ya Arsenal haijatoa tamko lolote kuhusu uhamisho wa Adebayor.
UEFA yapunguza adhabu za Drogba na Bosingwa
Chama cha Soka Ulaya, UEFA, kimewapunguzia adhabu Didier Drogba na Jose Bosingwa walizopewa baada ya utovu wa nidhamu dhidi ya Refa Tom Henning Ovrebo kutoka Norway baada ya mechi ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE iliyochezwa Stamford Bridge kati ya Chelsea na Barcelona ambayo Barca waliibuka washindi kwa goli la ugenini.
Drogba alifungiwa mechi 4 na sasa imepunguzwa hadi mechi 3 na Bosingwa amepunguziwa kutoka mechi 3 hadi 2.
Kupunguziwa adhabu hizi kunafuatia rufaa ya Wachezaji hao iliyofanywa leo na kuhudhuriwa na Wachezaji hao.
Wakati huo huo, Klabu ya Chelsea imetangaza imeongeza mkataba wao na Wafadhili wao Samsung hadi mwaka 2013.
Kampuni hiyo ya Elektroniki ilianza kuwa mfadhili wa Chelsea tangu mwaka 2005.

No comments:

Powered By Blogger