Saturday 18 July 2009

Gareth Barry amwambia Benitez anakosa heshima!
Kiungo mpya wa Manchester City, Gareth Barry, amemshambulia Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, na kumsema amekosa heshima kwa kutamka yeye ameichagua Man City badala ya Liverpool kwa uroho wa pesa tu.
Msimu uliokwisha Liverpool walitaka kumchukua Barry kutoka Aston Villa lakini Liverpool hawakuafiki dau walilolitaka Aston Villa.
Barry ambae pia huchezea Timu ya Taifa ya England amesema: ‘Ni dhahiri maneno ya Benitez ni kukosa heshima! Nadhani amechukizwa kwa kuwa sikwenda Liverpool! Liverpool walikuwa na kila uwezo kunichukua lakini wameona thamani yangu ndogo wakati Man City wamenithamini.’

No comments:

Powered By Blogger