Wednesday 15 July 2009

Fainali Copa Libertadores: Leo marudio Cruzeiro v Estudiantes!
Mechi ya pili ya Fainali ya Kombe la Klabu Bingwa za Nchi za Marekani ya Kusini, ambayo ni Fainali ya 50 ya Mashindano hayo maarufu kwa jina la COPA LIBERTADORES, leo itachezwa nchini Brazil baina ya Timu za Nchi Mahasimu Kisoka Argentina na Brazil , baada ya Klabu hizo za Estudiantes ya Argentina na Cruzeiro ya Brazil kutoka suluhu 0-0 kwenye mechi ya kwanza iliyochezwa wiki iliyokwisha.
Fainali hii inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.

Wachezaji wa Nigeria kupimwa kutambua umri!!
Wachezaji wa Nigeria watakaocheza Kombe la Dunia la Vijana chini ya miaka 17 itabidi wapimwe mifupa ili kuthibitisha umri wao katika Fainali hizo ambazo Nigeria ndio Wenyeji wa mashindano hayo yatakayochezwa kati ya Oktoba 24 na Novemba 15 mwaka huu.
Kumekuwa na tuhuma nyingi dhidi ya Nigeria katika mashindano mbalimbali ya kimataifa kwamba Nigeria huchezesha Wachezaji waliozidi umri.
Nigeria wameshatwaa Kombe hilo la Dunia la Vijana chini ya miaka 17 mara 3 katika miaka ya 1985, 1993 na 2007.
Melo ajiunga Juve!!
Kiungo kutoka Brazil alieng'ara sana kwenye michuano ya hivi karibuni ya Kombe la Mabara huko Afrika Kusini na kuiwezsha Brazil kutwaa Kombe hilo, Felipe Melo, amehamia Juventus kutoka Fiorentina kwa ada ya Euro Milioni 25.
Melo alikuwa akihusishwa sana na Klabu ya Arsenal na hasa baada ya kupigiwa debe na Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Gilberto Silva, ambao wote ndio Viungo wa sasa wa Brazil.

No comments:

Powered By Blogger