Monday 13 July 2009

Sir Alex: 'Hatununui mtu! Hizi mtu 3 tosha!' Owen apewa Jezi Namba 7!!

Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ametangaza kuwa hanunui Mchezaji yeyote tena kwa sababu Wachezaji Nyota wote Ulaya bei zao zimefumuka bila kukidhi thamani sahihi.

Sir Alex Ferguson amesema pia ingawa alishazoea kununua Wachezaji kwa bei mbaya kwa vile tu Klabu zinazouza Wachezaji hao zinajua fika wanawauzia Man U lakini 'sama' hii bei 'zimebomoa paa'!

Mpaka sasa Manchester United imenunua Wachezaji watatu tu ambao ni Michael Owen, Luis Antonio Valencia na Gabriel Obertan [pichani wakiwa na Ferguson].

Veterani Michael Owen amepewa Jezi Namba 7 ambayo kihistoria Manchester United waliivaa Wachezaji waliotukuka kama George Best, Bryan Robson, Eric Cantona na David Beckham.

Mchezaji wa mwisho kuivaa ni Ronaldo aliehamia Real Madrid.

Ferguson amenukuliwa akisema: 'Ni mwisho wa biashara yetu! Hadithi nyingine zote-sahau! Kila kona England na Ulaya, thamani ya Wachezaji imepasua paa! Hamna uhamisho wenye thamani ya kweli!'

Ferguson, akiwapoza Washabiki, akasisitiza: 'Tuna Kikosi imara. Kuondoka Mchezaji mmoja watu wasianze kuhamanika! Tumemruhusu aondoke na sisi tuna Kikosi kizuri! Nimeleta Chipukizi na Mkongwe Owen na mtaona akifunga magoli! Siku zote nilikuwa nikiwaambia Madifenda wangu tukicheza nae, msijiache mmesimama tu, atawaponyoka na kufunga, ni hatari huyu!'

Adebayor kwenda Man City???
Kuna uvumi mkubwa kuwa Mshambuliaji wa Arsenal, Emmanuel Adebayor kutoka Togo, yuko mbioni kujiunga na Manchester City iliyokosa kumsaini Mshambuliaji wa Cameroun Samuel Eto'o.

Inaelekea Manchester City wamewapiku AC Milan waliokuwa wakimwania kwa muda mrefu na hata Mchezaji mwenyewe kukiri, wakati fulani, kuwa AC Milan ni Timu nzuri.

Inategemewa Adebayor akihama, Meneja Arsene Wenger atamchukua Mshambuliaji toka Morocco Marouane Chamakh anaecheza Klabu ya Ufaransa Bordeaux ambae mwenyewe yuko tayari kutua Uwanjani Emirates.

No comments:

Powered By Blogger