Saturday 18 July 2009

Owen aipa ushindi Man U!!!
Michael Owen akianza mechi yake ya kwanza kwa Klabu yake mpya Manchester United amefunga bao lake la kwanza na la ushindi katika mechi ya kwanza katika ziara yao ya huko Asia kwa kuifunga Kombaini ya Malaysia kwenye Uwanja wa Bukit Jalil huko Kuala Lumpur kwa mabao 3-2.
Magoli mengine ya Man U yalifungwa na Rooney dakika ya 8 na Nani dakika ya 28.
Mpaka haftaimu Man U walikuwa mbele 2-1 lakini kosa kubwa la Kipa Ben Foster alieingia kipindi cha pili kushindwa kuzuia pasi aliyorudishiwa na mwenzake Gibson yaliwapa Malaysia bao la chee la kurudisha.
Ndipo Owen akafunga bao la 3 dakika ya 85 baada ya kazi nzuri ya Giggs.
Man U wanasafiri hadi Korea ya Kusini na Ijumaa ijayo watacheza na Klabu ya Korea FC Seoul.
Kikosi: Van der Sar; O'Shea, Ferdinand, Evans, Evra; Gibson, Scholes, Anderson, Nani; Rooney, Berbatov. Akiba: Foster, Neville, Brown, Owen, Giggs, Tosic, Fabio, Macheda

No comments:

Powered By Blogger