Friday 17 July 2009

David Beckham: ‘Terry hahami Chelsea!’
Ingawa Nahodha wa Chelsea na England, John Terry, anatakiwa sana na Manchester City, Nahodha wa zamani wa England, David Beckham, anaamini
Terry hawezi kuhama.
Inaaminika Man City imetoa ofa ya Pauni Milioni 35 kumnunua Mchezaji huyo ambae binafsi ameelekea anataka kuondoka.
Beckaham amedai: ‘ Sidhani JT atang’oka! Yeye ni Chelsea damu!’
Wakati anazungumza hilo, Beckham amesema: ‘ Wakati ule sikupenda kuhama Man U! Nilipoondoka sikupenda kuitazama Man U! Roho iliniuma sana! Niliamua mie ni Mchezaji Man U milele! Kwa miaka miaka mitatu nilipokuwa Real nilishindwa kuitazama Man U kwenye TV roho iliuma!’

No comments:

Powered By Blogger