Tuesday 14 July 2009

Benitez: 'Alonso aombe rasmi kama anaenda Real'
Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, amesema kuwa Kiungo wake Xabi Alonso anapaswa kuomba kwa maandishi ikiwa anataka kuhamia Real Madrid ili kila mtu ajue kwamba kweli anayo nia hiyo.
Inasemekana Alonso alimpigia simu Meneja huyo na kumwambia anataka kuhamia Real Madrid na Benitez akamtaka aandike barua.
Hata hivyo, Benitez amesisitiza ikiwa kweli Real wanamtaka Alonso basi lazima wailipe Liverpool Pauni Milioni 35 ingawa Real wametamka thamani ya Alonso haizidi Pauni Milioni 25.
Kocha mpya wa Real Madrid anaetoka Argentina, Manuel Pellegrini, ametamka: 'Si siri, tunamtaka Alonso lakini kumpata ni ishu nyingine!'

No comments:

Powered By Blogger