Saturday 18 July 2009

Barca na Inter zabadilishana Washambuliaji!!
Barcelona na Inter Milan wamefikia makubaliano ya kubadilishana Zlatan Ibrahimovic atakaenda Barca na Samuel Eto'o atakaekwenda Inter.
Pia, katika mpango huo Barca itaongeza pesa na kumtoa Kiungo wa zamani wa Arsenal Alex Hleb achezee Inter Milan kwa mkopo.
Habari hizi zimethibitishwa na Rais wa Barcelona, Joan Laporta, aliesema: ‘Makubaliano hayo yanategemea kuridhika kwa upande wa Ibrahimovic na Eto’o.’
Mshambuliaji Manucho kuondoka Man Utd
Manchester United imemruhusu Mshambuliaji kutoka Angola Manucho [pichani akiwa na Ronaldo]kujiunga na Klabu ya Spain Real Valladolid kwa mkataba wa miaka mitano.
Manucho, miaka 26, amekuwa Man U kwa miezi 18 na alicheza mechi moja tu ya Ligi Kuu na kushindwa kupata namba na muda mwingi amekuwa akicheza Klabu nyingine kwa mkopo.
Alipojiunga tu na Man U akapelekwa Klabu ya Ugiriki Panathinaikos kwa mkopo na msimu uliokwisha alicheza Hull City pia kwa mkopo.
Hargreaves akaribia kurudi Uwanjani Man U
Mchezaji wa Manchester United Owen Hargreaves huenda akaanza kuonekana tena uwanjani kuanzia mwezi Septemba kufuatana na maelezo ya Bosi Sir Alex Ferguson.
Kiungo huyo hajaonekana uwanjani tangu mwanzoni mwa msimu uliokwisha kwa kusumbuliwa na matatizo ya magoti na kmfanya afanye opersheni kila goti huko Marekani.
Hargreaves, miaka 28, hayumo kwenye Kikosi cha Man U kilichopo ziarani Asia lakini huenda akajiunga na wenzake watakapokuwa Ujerumani kugombea Kombe la Audi wiki mbili zijazo.
Katika Kombe hilo Man U watacheza na Boca Juniors ya Argentina.
Mechi ya mwisho ya Hargreaves ilikuwa Septemba 21, 2008 Man U ilipocheza na Chelsea huko Stamford Bridge na kutoka suluhu 1-1 kwenye Ligi Kuu.

No comments:

Powered By Blogger