Monday 13 July 2009

Tevez yuko Man City!!
Kuna taarifa zimeibuka na kuthibitishwa kuwa Carlos Tevez amejiunga na Wapinzani wa Manchester United, Manchester City.
Meneja wa Manchester City, Mark Hughes, amethibitisha habari hizo na kushangilia usajili huo kwa kumsifia Tevez kuwa ni Mchezaji wa Kimataifa wa kiwango cha juu.
Tevez anategemewa kupimwa afya kabla ya kukamilisha taratibu za usajili.
Tevez alichukuliwa na Manchester United kwa mkopo toka Kampuni inayommiliki baada ya kucheza West Ham na alikaa Man U kwa miaka miwili.
Man U walikuwa tayari kulipa pesa za kumnunua Tevez na pia walishampa ofa ya mkataba wa miaka mitano na mshahara mkubwa tu ambao ungemfanya Tevez awe mmoja wa Wachezaji wa Man U wanaolipwa donge nono sana, lakini Tevez aligoma kwa madai kuwa msimu uliokwisha alidharauliwa kwa kutopangwa mara kwa mara.
Mkataba wa Tevez na Manchester United ulimalizika Juni 30.

No comments:

Powered By Blogger