Thursday 16 July 2009

Ronaldo: 'Owen anastahili Jezi Namba 7 Man U!'
Cristiano Ronaldo anaamini Michael Owen ni mrithi bora wa Jezi Namba 7 aliyoivaa yeye alipokuwa Manchester United.
Jezi hiyo kihistoria imekuwa ikivaliwa na Wachezaji mahiri sana katika Klabu ya Manchester United na waliowahi kuivaa huko nyuma ni pamoja na Wachezaji walioacha historia kubwa kama George Best, Bryan Robson, Eric Cantona, David Beckham na wa mwisho ni yeye Ronaldo.
Ronaldo ametamka: 'Michael Owen ni Mchezaji mzoefu. Amecheza Klabu kubwa. Atashinda kila kitu akiwa Man U. Yupo kwenye Klabu murua sana na yeye ni Mchezaji Bora. Ni uamuzi mzuri kumpa Jezi Namba 7!'
Michael Owen amesainiwa hivi karibuni na Manchester United bila ya ada ya uhamisho kwa kuwa alikuwa Mchezaji huru baada ya mkataba wake na Newcastle kumalizika Juni 30.
Winga Downing aenda Villa kwa Pauni Milioni 12!
Winga wa Timu iliyoporomoka Daraja Middlesbrough, Stewart Downing, ambae pia yumo Kikosi cha England, amehamia Aston Villa kwa kitita cha Pauni Milioni 12.
Downing, umri miaka 24, ni Mchezaji wa kwanza kusainiwa na Meneja wa Aston Villa Martin O'Neill kwa ajili ya msimu ujao.
Downing aliwahi kuomba kuihama Middlesbrough mwezi Januari lakini akagomewa lakini baada ya Klabu hiyo kuporomoka Daraja Mwenyekiti wake Steve Gibson alitangaza hawezi kumzuia Mchezaji yeyote kuihama Klabu hiyo.

No comments:

Powered By Blogger