Tuesday 14 July 2009

Fergie atunukiwa Digrii!!
Meneja wa Mabingwa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ametunukiwa Digrii ya Heshima na Chuo Kikuu cha Mjini Manchester kwa mchango wake kwa Jiji la Manchester.
Sir Alex Ferguson, aliezaliwa Desemba 31, mwaka 1941, alijiunga na Klabu ya Manchester United mwaka 1986 na kuiwezesha kutwaa Vikombe vingi kupita Meneja yeyote katika historia ya soka huko Uingereza.
Mwaka 1999, Malkia wa Uingereza alimtunuku heshima ya kuitwa 'Sir' kwa kuiwezesha Manchester United kutwaa Vikombe vitatu kwa mpigo, yaani, FA Cup, Ligi Kuu na Kombe la Klabu Bingwa Ulaya.
Vilevile, Sir Alex Ferguson anayo heshima ya kupewa Tuzo ya Uhuru wa Mji wa Aberdeen huko Scotland baada ya kuiwezesha Klabu ya Aberdeen ya huko Scotland katika miaka ya 1980 kuvunja himaya ya Klabu Vigogo za huko, Celtic na Rangers, na kutwaa Vikombe kadhaa likiwemo Kombe la Washindi la Ulaya walipowafunga Real Madrid mabao 2-1 katika Fainali iliyochezwa Mei 11, mwaka 1983.

No comments:

Powered By Blogger