Saturday 18 July 2009

Fulham kucheza na FK Vetra au HJK Helsinki EUROPA LEAGUE
Klabu ya Ligi Kuu England, Fulham, itaanza Raundi ya Tatu ya Mtoano ya Kombe jipya huko Ulaya liitwalo EUROPA LEAGUE kwa kucheza na mshindi kati ya FK Vetra ya Lithuania au HJK Helsinki ya Finland.
Timu hizo zimeshacheza mechi ya kwanza na HJK Helsinki waliishinda FK Vetra ugenini bao 1-0 na watarudiana wiki ijayo na mshindi atapambana Fulham tarehe 30 Julai nyumbani na marudiano yatachezwa Craven Cottage nyumbani kwa Fulham tarehe 6 Agosti.
Fulham imeingizwa EUROPA LEAGUE baada ya kumaliza nafasi ya 7 kwenye Ligi Kuu England pamoja na Everton na Aston Villa zilizomaliza nafasi ya tano na ya sita lakini Everton na Aston Villa zitaanza kucheza Raundi inayofuata.
Man U wamyakua Kijana toka Senegal!!
Klabu za Manchester United na Molde F.K. ya Norway zimethibitisha kuwa zimekubaliana kuhusu uhamisho wa Mame Biram Diouf , miaka 21, raia wa Senegal, kwenda Man U kwa dau ambao halikutangazwa.
Mame atapimwa afya yake huko Manchester wiki ijayo lakini ataendela kuichezea Molde hadi Januari mwakani ili amalizie msimu wa Norway.
Akiongea na Waandishi wa Habari huko Kuala Lumpur, Malaysia ambako Manchester United wako ziarani, Sir Alex Ferguson alisema: ‘Tumekuwa tukimfuatalia kwa miaka miwili sasa! Tulikuwa hatuna nia ya kusajili mtu lakini kuhusu Mame imebidi tumchukue sasa kwa vile Klabu nyingi zimetoa ofa kwake!’
Mpaka leo, baada ya kucheza Klabu ya Molde, klabu ambayo Ole Gunnar Solskjaerpia alikuwa akiechezea, Mame ameshafunga mabao 38 katika mechi 73 na msimu huu katika mechi 21 ameshafunga mabao 17.
Mame anaichezea Timu ya Taifa ya Vijana ya Senegal.

No comments:

Powered By Blogger