Monday 20 July 2009

Alonso akiri Real kunapendeza!!!
Kiungo wa Liverpool, Xabi Alonso ambae ashabatukiwa na Meneja wake Rafa Benitez kuwa akitaka uhamisho kwenda Real Madrid basi lazima aandike barua rasmi kuomba, amekiri kuwa anavutiwa na kujiunga na Real.
Alonso amesema: ‘Mchezaji hujisikia vizuri ukitakiwa na Real hasa ukizingatia wakati huu nilio. Lakini hili ni suala la pande tatu nikiwemo mimi.’
Alonso ameongeza kuwa akiwa Nchini Austria ambako Liverpool wamepiga kambi ya mazoezi na kuwa ziarani huko ataongea na Benitez kuhusu uhamisho.
Mido aendelea kutwangwa faini kadri anavyochelewa kurudi Boro!!
Mchezaji wa Misri, Mido, ambae mpaka sasa wiki mbili zimepita na bado hajaripoti kwenye Timu yake Middlesbrough ambayo imeshuka Daraja kutoka Ligi Kuu England msimu uliokwisha, ameendelea kukung’utwa faini zaidi na Klabu hiyo.
Meneja wa Boro, Gareth Southgate, amesema: ‘Mido lazima arudi na kufanya mazoezi na sisi. Klabu haiwezi kumlipa mtu yeyote kama hayupo na sisi!’
Mpaka sasa Mido, ambae alimaliza msimu uliokwisha akichezea Wigan kwa mkopo, ameshapigwa faini ya mshahara wa wiki mbili.
Mido alisainiwa na Boro mwaka 2007 kutoka Tottenham Hotspurs kwa Pauni Milioni 6.
Guardiola hamtaki Eto'o!!
Kocha wa Barcelona Pep Guardiola, ambae msimu uliokwisha alimweka Samuel Eto'o kwenye listi ya uhamisho, amesema lazima Eto’o aondoke.
Barcelona na Inter Milan zipo kwenye mazungumzo ili zifikie makubaliano ya kubadilishana Et’oo na Zlatan Ibrahimovic.
Guardiola amesema: ‘Nina imani kitu bora kwa Barca ni kuondoka kwa Eto’o. Siko hapa kumbadili mtu tabia ila niko hapa kufanya uamuzi. Umefika wakati kubadilika kwa ajili ya msimu ujao.’

No comments:

Powered By Blogger