Monday 20 July 2009

Owen afunga tena!!
Michael Owen akicheza mechi yake ya pili leo akiwa na Jezi Namba 7 ya Manchester United amefunga bao kwa mara nyingine tena kwenye mechi Man U waliyowafunga wenyeji wao Malasyia mjini Kuala Lumpur bao 2-0.
Bao la kwanza la Manchester United lilifungwa na Chipukizi Macheda dakika ya 11 na la pili alipachika Owen dakika ya 13.
Katika mechi hiyo ya kirafiki kila Timu ilifanya mabadiliko ya Wachezaji wengi mno huku Man U ikiwaingiza katika kipindi cha pili Kipa Kuszczak, Rio Ferdinand, Nani, Berbatov, Scholes, Anderson, Gibson, O’Shea, Evra na Rooney.
Sasa Man U wanaelekea Korea ya Kusini kucheza na Klabu ya FC Seoul siku ya Ijumaa.
Kikosi cha Man U kilichoanza ni: Foster; Neville, Brown, Evans, Fabio; Fletcher, Carrick, Giggs, Tosic; Owen, Macheda.

No comments:

Powered By Blogger