Sunday 19 July 2009

Carlo Ancelotti: ‘Terry ni alama ya Chelsea!!’
Meneja mpya wa Chelsea Carlo Ancelotti amesema Nahodha wa Timu hiyo John Terry ni ‘alama’ ya Klabu hiyo na ana uhakika wa zaidi ya aslimia mia moja kuwa Terry atabaki Stamford Bridge.
Manchester City, ikitumia miguvu ya mipesa toka kwa Wamiliki wake Matajiri toka Koo ya Kifalme kutoka huko Abu Dhabi, Falme za Nchi za Kiarabu, imekuwa ikimsaka Terry kwa udi na uvumba.
Akiongea baada ya Chelsea, wakiwa ziarani Marekani, kuwafunga Seattle Sounders mabao 2-0 mjini Seattle, Kocha huyo Mtaliano alisema: ‘Terry ni mwungwana. Hawezi kuhama Timu ambayo yeye ni nguzo!’
Owen: ‘Nitamudu shinikizo la kuwa Man U!!’
Baada ya kufungua kitabu chake cha magoli kwa Timu yake mpya katika mechi yake ya kwanza tu alipofunga bao la 3 na la ushindi wakati Manchester United walipowapiga wenyeji wao Malaysia kwa bao 3-2 mjini Kuala Lumpur, Michael Owen ametamka hana wasiwasi na atamudu kuziba pengo la Ronaldo akishirikiana na wenzaki kina Giggs na Rooney.
Owen ametamka: ‘Ni nafasi kubwa kwangu kuonyesha uwezo na pia kuwa naweza kumudu shinikizo. Kupewa Jezi Namba 7 iliyovaliwa na Wachezaji bora ni shinikizo kubwa kwangu lakini nitaitumikia ipasavyo! Sir Alex Ferguson alinitaka nivae Jezi hiyo na alitaka Mchezaji anaeweza kuimudu Jezi hiyo yenye historia kubwa kwa Man U! Nikamjibu naweza!’

No comments:

Powered By Blogger