Tuesday 21 July 2009

Arsenal yakumbwa na balaa, Nasri avunjika mguu!!
Kiungo wa Arsenal, Samir Nasri amevunjika mguu katika mechi ya mazoezi huko Nchini Austria ambako Arsenal wameenda kupiga kambi ya mazoezi ya kujitayarisha na msimu mpya unaoanza Agosti 15.
Nasri, miaka 22, alikimbizwa hospitalini na Madaktari wamekadiria atakuwa nje ya uwanja kwa kati ya miezi miwili mpaka mitatu.
Klabu yake Arsenal imethibitisha habari hizo kupitia tovuti yake.
Portsmouth yanunuliwa na Tajiri toka Dubai!
Portsmouth imethibitisha kuwa Sulaiman Al Fahim ndie Mwenyekiti mpya wa Klabu hiyo baada ya kukubaliwa kuinunua na Wasimamizi wa Ligi Kuu England ambao siku hizi wameanzisha mfumo mpya wa kuhakikisha wanaozinunua Klabu za Ligi Kuu wana sifa wa kuzimiliki Klabu hizo.
Al Fahim, anaetoka Dubai, Falme ya Nchi za Kiarabu, ndie alieongoza ununuzi wa Manchester City alipowawakilisha Koo ya Kifalme ya Abu Dhabi katika ununuzi wake lakini safari hii ni yeye binafsi alieinunua Portsmouth.
Al Fahim ameinunua Portsmouth kutoka kwa Alexandre Gavdamak.
Real Madrid, Ronaldo akiwa ndani, waifunga Timu ndogo ya huko Ireland kwa mbinde!!!
Kwa mara ya kwanza Christiano Ronaldo amevaa Jezi nyeupe ya Real Madrid na kucheza dakika 45 za kwanza lakini alikuwa Mchezaji mpya mwenzake kutoka Ufaransa Karim Benzema aliefunga goli la ushindi dakika 3 kabla mpira kumalizika pale vigogo Real Mdrid walipoitungua Timu ndogo ya Ireland Shamrock Rovers bao 1-0.
VFL Wolfsburg 1 v Werder Bremen 2!
Bremen yatwaa Super Cup!!
Kombe liitwalo Super Cup huko Ujerumani jana lilikwenda kwa Mabingwa wa Kombe la Ujerumani Werder Bremen walipowafunga Mabingwa wa Ujerumani Vfl Wolfsburg mabao 2-1.
Bremen walitangulia kufunga dakika ya 20 kwa Per Mertesacker kufunga lakini Wolfsburg walisawazisha dakika ya 67 kupitia Mchezaji wao hatari kutoka Brazil Grafite dakika ya 67.
Lakini alikuwa Clemens Fritz kwenye dakika ya 81 alipowapa furaha Werder Bremen kwa kupachika bao la pili na la ushindi.

No comments:

Powered By Blogger