Thursday 23 July 2009

Spurs yanyakua Vijana Naughton na Walker
Tottenham imewanunua Vijana wawili kutoka Sheffield United Timu inayocheza daraja la Chini ya Ligi kuu yaani Coca Cola Championship.
Vijana hao ambao wote ni Walinzi ni Kyle Naughton na Kyle Walker wamechukuliwa kwa jumla ya Pauni Milioni 10 ingawa hilo halikuthibitishwa.
Wakati Walker, miaka 19, atabaki Sheffield United kwa mkopo Naughton, miaka 20, atakuwepo Klabu yake mpya akigombea namba na kina Corluka na Hutton ambao wote huchezea nafasi moja.
Mikel ajikita Chelsea
Kiungo wa Chelsea anaetoka Nigeria, John Mikel Obi, miaka 22, amesaini mkataba mpya wa miaka mitano hapo Stamford Bridge.
Mikel alijiunga Chelsea akitokea Klabu ya Norway Lyn Oslo mwaka 2006 huku kukiwa na mvutano na Manchester United ambao ndio walimsaini kwanza na mzozo huo ulifika mpaka FIFA na ikabidi Chelsea wailipe Manchester United pauni Milioni 12.
Akizungumzia mkataba huu Mikel alitamka: ‘Ni rahisi kusaini kwani nina furaha hapa!’
Akiwa Chelsea, Mikel ashacheza chini ya Mameneja Jose Mourinho, Avram Grant, Luiz Felipe Scolari ,Guus Hiddink na sasa Carlo Ancelotti.
Gerrard alikiri kupiga ngumi 3!!
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, alikiri kumpiga Marcus McGee ngumi tatu lakini ni moja tu ndio ilitua usoni kufuatana stetimenti aliyoandika Polisi na kusomwa Mahakamani katika kesi dhidi yake na Wenzake 6 wanaotuhumiwa kumshambulia na kumjeruhi Marcus McGee Desemba 29 mwaka jana.
Gerrard mwenyewe anategemewa kutoa ushahidi wake leo.
Liverpool 1 Thailand 1
Mchezaji alietoka benchi na kuingizwa kipindi cha pili Sutee Suksomkit alifunga bao la kusawazisha kwa Thailand na kulazimisha sare ya 1-1 na Liverpool katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Bangkok, Thailand.
Bao la Liverpool, iliyosheheni Masupastaa, lilifungwa na Ryan Babel dakika ya 6.
Thailand inafundishwa na Mchezaji wa zamani wa England aliewahi pia kuwa Meneja wa Sunderland Peter Reid.
Hii ni suluhu ya pili mfululizo kwa Liverpool iliyo katika maandalizi ya msimu mpya.
Liverpool Jumapili inacheza na Timu ya Taifa ya Singapore
.

No comments:

Powered By Blogger