Saturday 25 July 2009

Gerrard akwepa Lupango!!!
Nahodha wa Liverpool na Kiungo wa England, Steven Gerrard, amepatikana kutokuwa na hatia katika kesi ya kushambulia na kumjeruhi Marcus McGee Desemba 29 mwaka jana huko Southport.
Ingawa Gerrard alikiri kumpiga ngumi McGee na kujitetea kuwa alifanya hivyo ili kujihami, Wazee wa Baraza Mahakamani wamekubali kauli yake na kumwona hana hatia.
Akiongea baada ya kesi kumalizika, Gerrard alisema: 'Nimefurahi na sasa haya yote yamepita!’
Adebayor adai ameuzwa kwani Arsenal hawana pesa!!
Emmanuel Adebayor amedai Arsenal ilimuuza kwa Manchester City kwa sababu walikuwa wanataka fedha.
Adebayor amenunuliwa na Man City kwa Pauni Milioni 25.
Adebayor ametamka: ‘Niliporudi toka likizo Wakala wangu akaniambia Klabu inataka kuzungumza na mimi. Ndipo Wenger akaniambia wamefikia makubaliano na Klabu nyingine kuhusu mimi. Nadhani walitaka pesa ila namshkuru Wenger kwa kunifikisha hapa!’
Matokeo mechi za kirafiki:
-Celtic 5 El Ahly 0
-Tottenham 1 Barcelona 1
-Chelsea 2 AC Milan 1
-FC Koln 0 Bayern Munich 2
-FC Seoul 2 Manchester United 3

No comments:

Powered By Blogger