Friday 24 July 2009

Kepteni wa Korea ndani ya Man U kwao Korea!
Park Ji-sung Ijumaa atakuwa nyumbani lakini si kwa Timu yake ya Taifa ya Korea ambayo yeye ni Kepteni bali ni Klabu yake Manchester United wakati Man U itakapocheza na FC Seoul kwenye mechi ya kirafiki.

Hii ni ziara ya pili kwa Man U Nchini Korea lakini itakuwa ni mechi ya kwanza kwa Park kucheza kwao akivaa Jezi ya Man U kwa sababu miaka miwili iliyopita Man U walipozuru huko Park alikuwa kaumia goti na hakucheza.

Sir Alex Ferguson akiwa na furaha kuhusu Park alieleza: 'Kijana wa nyumbani Ji-sung akiacha Nchi yake kuchezea Man U ni furaha lakini kufanikiwa na kuwa staa kama yeye bila shaka nyumbani atapokewa kwa shangwe! Pia yeye, kama Nahodha wa Timu ya Taifa, mapokezi yatakuwa bora! Korea ni Nchi ya soka, amerudi atapokewa vyema! Huyu ni mfano mwema!'

No comments:

Powered By Blogger