Monday 20 July 2009

Liverpool wafungwa huko Austria!
Huku wakiandamwa na kashfa ya Nahodha wao, Steven Gerrard, kutinga Mahakamani na shinikizo la Xabi Alonso kuhusishwa na Real Madrid, Liverpool jana walipigwa kimoja na Rapid Vienna ya Austria kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa Austria ambako Liverpool wako ziarani.
Hii ni mechi ya pili ya kirafiki kwa Liverpool wanaojitayarisha kwa mwanzo wa msimu mpya wa Ligi Kuu England baada ya kutoka suluhu 0-0 na Club St Gallen ya Switzerland Jumatano wiki iliyopita.
Bao la Rapid Vienna lilifungwa na Nahodha wao Steffen Hofmann dakika ya 58 kwa frikiki bomba.
Jumatano Liverpool watakuwa huko Asia Nchini Thailand kucheza na Timu ya Taifa ya Thailand.

No comments:

Powered By Blogger