Monday 20 July 2009

Gerrard apanda kizimbani leo!
Nahodha wa Liverpool na Kiungo wa England, Steven Gerrard, leo ametinga Mahakamani ili kusikilizwa kesi yake anayotuhumiwa yeye na wenzake 6 ya kumshambulia na kumjeruhi Marcus McGee kwenye Naitiklabu usiku wa Desemba 29 mwaka jana huko Liverpool.
Kufuatana malumbano ya kisheria na pia kutoteuliwa Wazee wa Mahakamani, kesi hiyo imeahirishwa hadi kesho Jumanne na inategemewa kesi hiyo itadumu wiki 2 au 3 mpaka kumalizika.
Gerrard, miaka 29, amekanusha mashtaka hayo ambayo ameunganishwa na Kipa wa Klabu ndogo iitwayo Accrington Stanley anaeitwa Ian Dunbavin, 28, na pia Kiungo wa Timu hiyo Robert Grant, 18. Wengine ni John Doran, 29, Ian Smith, 19, John McGrattan, 33, na Paul McGrattan, 31.
Inaaminika genge hilo la Gerrard lilikuwa linasheherekea ushindi wa Liverpool wa siku hiyo walipoibamiza Newcastle bao 5-1.

No comments:

Powered By Blogger