Wednesday 22 July 2009

Gerrard kumkabili Pilato pekee, Wenzake waungama na kusubiri hukumu!!!!
Nahodha wa Liverpool na Mchezaji wa Timu ya Taifa, Steven Gerrard, peke yake atasimama kizimbani ili kesi yake kuendelea kusikilizwa baada ya Washitakiwa wenzake wote 6 kukubali makosa na hivyo kungoja hukumu tu ya kosa la kumpiga na kumjeruhi Marcus McGee Desemba 29 mwaka jana kwenye Naitiklabu Lounge Inn huko Southport.
Gerrard amekana mashitaka hayo na hivyo kesi inaendelea kunguruma kwake tu na Mwendesha Mashtaka alisimama na kuelezea korti nini kilijiri huku mikanda ya video ya kamera za ulinzi ikionyeshwa.
Mwendesha Mashtaka huyo, David Turner, aliieleza Mahakama: ‘Ugomvi ulianza pale Gerrard alipotaka apewe kadi inayoongoza CD za muziki. McGee alipogoma kumpa, Gerrard akachukia.
Baada ya dakika 6 hivi, Gerrard, akamrudia McGee na kumtukana kisha Mshtakiwa mwenzake Gerrard akaja na kumsukuma McGee na kumpiga kipepsi na ndipo Gerrard akanza kuvurumisha masumbwi mithili ya Bondia!’
Turner akaongeza: ‘Swali zito hapa ni je Gerrard alikuwa akijihami? Gerrard ni Mchezaji Bora Duniani! Anayo heshima ya kuwa Nahodha wa Liverpool na kuichezea Timu ya Taifa ya England! Ni nyota yeye aliezaliwa Liverpool na hapa Liverpool Gerrard ni shujaa! Hatusemi Gerrard ni mtu mwenye kiburi! Hatusemi ni mbabe! Tunachosema hapa usiku ule Gerrard alipandwa hasira na kuanza kumshambulia mtu bila sababu! Amejiangusha yeye mwenyewe binafsi!’
Kesi inaendelea.

No comments:

Powered By Blogger