Thursday 29 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Robinho kurudi Man City
Bosi wa Manchester City Roberto Mancini amesema Robinho atarudi tena Klabuni hapo hivi karibuni baada ya kumalizika Mkataba wake wa mkopo na Santos ya huko kwao Brazil.
Mancini amesema yeye hana tatizo kumkaribisha tena Robinho ambae alilazimisha kurudi kwao Brazil kwa vile hakuwa na furaha hapo Manchester.
Baada ya kurudi Santos, Robinho aliibuka na fomu mpya na pia kung’ara na Brazil huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia.
Anelka alishitaki Gazeti kwa kumdhalilisha
Nikolas Anelka, ambae alitimuliwa toka Kikosi cha Ufaransa huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia, yuko mbioni kufungua mashitaka kwa Gazeti la kila siku la huko Ufaransa la Michezo, L’Equipe, kwa kumchafulia jina katika stori ya Gazeti kuwa alimtukana aliekuwa Meneja wa Ufarnasa Raymond Domenech.
Ingawa Anelka hajakana kuwa alimtukana Domenech wakati wa hafutaimu wa Mechi ya Kombe la Dunia Juni 17 dhidi ya Mexico, amedai kuwa GAzeti L’Equipe limepotosha maneno yake.
Wachezaji wengine wa Ufaransa waliokuwa huko Afrika Kusini wakati wa sakata la Anelka, akiwemo Thierry Henry, wamedai L’Equipe limetia chumvi mno.
Hata hivyo Gazeti hilo linadai stori yao ni sahihi

No comments:

Powered By Blogger