Monday 26 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Raul kuondoka Real
Baada ya Miaka 18 ya utumishi kwa Real Madrid, Straika Raul amedai yuko njiani kuondoka na huenda akaangukia England kwenye Ligi Kuu.
Raul, Miaka 33, alitegemewa kujiunga na Klabu ya Ujerumani Schalke lakini mwenyewe ameziruka habari hizo.
Katika Mechi 741 alizoichezea Real, Raul alifunga mabao 323 na ameichezea Spain Mechi 102 na kufunga bao 44.
Raul alianza kuichezea Timu ya Kwanza ya Real Mwaka 1994 akiwa na Miaka 17 na alijiunga hapo Mwaka 1992.
Akiwa na Real ameweza kunyakua Ubingwa wa Ulaya mara 3 na La Liga mara 6.
Raul amesema baada ya siku chache atajua kama atacheza Bundesliga au Ligi Kuu England.
Ripoti ya Majeruhi wa Man United
Wakati Kikosi cha Manchester United kipo ziarani huko Marekani na baadae wataenda Mexico kwa mechi kadhaa, Wachezaji kadhaa wamebaki huko Manchester wakifanya mazoezi binafsi baada ya kupona maumivu yao.
Nahodha Gary Neville na Antonio Valencia wameanza mazoezi ya nguvu. Rio Ferdinand na Michael wameanza mazoezi mepesi.
Kuhusu majeruhi wa muda mrefu Anderson na Owen Hargreaves, Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amedokeza kuwa Anderson, alieumia goti Mwezi Februari Mwaka huu, anategemewa kuonekana Septemba na Owen Hargreaves ataendelea kubaki Marekani kwa Daktari aliempasua magoti yake mawili huko nyuma hadi waridhike na hali yake.
Man United yafungwa Marekani
Jana katika Uwanja wa Arrowhead, Kansas City, Marekani, Manchester United ilifungwa bao 2-1 na Kansas City Wizards.
Kansas City Wizards walifunga bao lao la kwanza dakika ya 11 kwa bao la David Arnaud na dakika ya 39 walipata pigo pale Jimmy Conrad alipotolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Berbatov aliisawazishia Man United kwa penalti dakika ya 41 lakini dakika mbili baadae Kei Kamara alipachika bao la pili na la ushindi kwa Kansas City Wizards.
Man United wanasafiri kwenda Jijini Houston kucheza na Mastaa wa Ligi ya huko Marekani MLS hapo Jumatano Julai 28.

No comments:

Powered By Blogger