Thursday 29 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com


Man United 5 MLS All Stars 2
• Chicharito acheza mara ya kwanza na kufunga!
Mchezaji mpya wa Manchester United kutoka Mexico, Javier Hernandez aka Chicharito, jana alicheza mechi yake ya kwanza na kumudu kufunga bao katika ushindi wa 5-2 wa Man United dhidi ya MLS All Stars ambayo ni Kombaini ya Wachezaji wa Ligi ya huko Marekani MLS.
Mechi hiyo ilichezwa mbele ya Mashabiki 71,000 Uwanjani Reliant, Houston.
Macheda ndie alieipatia Man United bao la kwanza sekunde ya 22 tu baada ya kuinasa pasi ya Beki Kevin Alston kwa Kipa wake.
Macheda aliongeza bao la pili kwa kichwa kufuatia kona ya Nani.
Dakika ya 63, MLS All Stars walipata bao kupitia Brian Ching lakini Man United wakaongeza bao mbili Wafungaji wakiwa Darron Gibson na Cleverly.
Chichariti alifunga bao lake la kwanza kwa Man United dakika ya 84 baada ya pande tamu la Fletcher.
MLS All Stars walipata bao lao la pili dakika ya 90 Mfungaji akiwa De Rosario.
Vikosi:
Manchester United: Van der Sar; Rafael, Brown, J Evans, Fábio (Scholes, 72); O'Shea; Obertan (Cleverley, 23), Fletcher, Giggs (Gibson, 52), Nani (Hernández, 62); Macheda (Welbeck, 62).
MLS All-Stars: Ricketts (Rimando); Alston (De Rosario,), Olave (Gonzalez, ht), Marshall (Conde, 63), Pearce (Donovan, 74); Joseph (Davis, 74); Le Toux (Convey,), Morales (Moreno, 63), Schelotto (Ferreira,), Pappa (Larentowicz,); Angel (Ching,).
Maradona alaumu usaliti!
Baada ya kukosa kuendelea kuwa Kocha wa Argentina, Diego Maradona, ameilaumu AFA, Chama cha Soka cha Argentina, kwa kusema uongo na kuwa wasaliti.
Maradona pia alimlaumu Meneja wa Timu ya Brazil, Carlos Bilardo, kwa kula njama yeye asipewe Ukocha Argentina.
Maradona aligoma kutii amri ya AFA ya kumtaka awaache baadhi ya Wasaidizi wake ikiwa atataka Mkataba mpya na hivyo AFA ililazimika kumtema.
Pia Maradona amedai Rais wa AFA, Grondona alimdangaya.
Kocha wa Timu ya Taifa ya Vijana wa Chini ya Miaka 20, Sergio Batista, ndie ameteuliwa kuwa Kocha wa Muda wa Argentina.
Fulham kumtangaza Mark Hughes Meneja mpya
Fulham inategemewa kumtangaza Mark Hughes kuwa Meneja mpya ndani ya Masaa 48 yajayo kuchukua nafasi ya Roy Hodgson aliehamia Liverpool.
Mark Hughes alitimuliwa kutoka Manchester City Desemba 2009 na kabla aliwahi kuwa Meneja wa Blackburn Rovers na Timu ya Taifa ya Wales.
Serie A kuanza Agosti 28
Mabingwa Watetezi wa Serie A huko Italia, Inter Milan, ambao pia ni Mabingwa wa Ulaya, wataanza kampeni yao ya utetezi wa Ubingwa wao kwa mechi ugenini dhidi ya Bologna.
Mechi za Wikendi ya Agosti 28 na 29:
Bari v Juventus
Chievo v Catania
Milan v Lecce
Parma v Brescia
Roma v Cesena
Sampdoria v Lazio
Uudinese v Genoa
Palermo v Cagliari
Bologna v Inter
Fiorentina v Napoli

No comments:

Powered By Blogger