Thursday 29 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

WATAHAMA, HAWAHAMI?
1. Fernando Torres
Ingawa fomu yake imeshuka kwa muda sasa, Torres anaendelea kuhusishwa na kuihama Liverpool huku Chelsea na Manchester City zikitajwa kama Timu ambazo atajiunga nazo.
Lakini Meneja wa Liverpool, Roy Hodgson, amepuuza habari hizo na kudai Torres anabaki Liverpool.
2. Cesc Fabregas
Bado kuna mvutano kati ya Barcelona na Arsenal kuhusu Nahodha huyu wa Arsenal.
Barcelona walishatoa ofa ya Pauni Milioni 29 na ikakataliwa na Ze Gunners na sasa Arsenal haitaki kuzungumza lolote kuhusu Fabregas ambae mwenyewe alishaonyesha nia ya kurudi Barca ambako ndiko alikoanzia Soka.
3. Javier Mascherano
Kiungo huyu kutoka Argentina ameshatamka bayana anataka kuihama Liverpool.
Mascherano anataka aende Inter Milan ili aungane tena na Meneja Rafael Benitez.
4. Mario Balotelli
Kuna kila dalili Supa Mario yuko mbioni kujiunga na Manchester City.
Kocha wa Man City, Roberto Mancini, anamtaka Chipukizi huyu kutoka Italia Klabu ya Inter Milan kwa udi na uvumba.
5. James Milner
Kuna mvutano wa dau la uhamisho kutoka Aston Villa kwenda Manchester City kwa Kiungo huyu Mwenye Miaka 24 huku Man City wakitoa ofa ya Pauni Milioni 24 lakini Villa wanataka Milioni 30.
6. Luis Suarez
Tottenham ndio wameonyesha nia ya kumchota mbaya huyu wa Ghana kutoka Uruguay ambae alisababisha Ghana itolewe Kombe la Dunia huko Afrika Kusini alipodaka mpira na kuwanyima Ghana bao la wazi.
Klabu yake Ajax Amsterdam ya Uholanzi inasemekana inataka Pauni Milioni 30.
7. Ricardo Carvalho
Beki huyu Mkongwe toka Ureno anataka kwenda Real Madrid ili kuungana tena na Meneja wake wa zamani huko Porto na Chelsea, Jose Mourinho.
8. Rafael van Der Vaart
Kiungo huyu wa Uholanzi hana namba ya kudumu huko Real Madrid na hilo limemfanya atake kuhama na Klabu za Liverpool na Chelsea ndizo zinamwania.
9. Mesut Ozil
Ni mmoja wa Wachezaji waliong’ara mno huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia akiwa na Ujerumani na kuna msululu wa Klabu zinazodaiwa kumwania ingawa Tottenham ndio ipo mbele. Nyingine ni Arsenal, Manchester United na Real Madrid.
Klabu yake Werder Bremen inataka Pauni Milioni 15.
10. Sami Khedira
Kiungo huyu wa Ujerumani ni Mchezaji mwingine aliewika huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia na Real Madrid ndio wanaotegemewa sana kumnasa kwa uhamisho wa Pauni Milioni 15.
UEFA CHAMPIONS LIGI: Raundi ya 3 Mtoano
MATOKEO Mechi za Jumatano Julai 28
Aktobe [Kazakstan] 1 Hapoel Tel-Aviv FC [Israel] 0
FC BATE Borisov [Belarus] 0 FC Kobenhavn [Denmark] 0
FC Sheriff Tiraspol [Moldova] 1 NK Dinamo Zagreb [Croatia] 1
Debreceni VSC [Hungary] 0 FC Basel 1893 [Switzerland] 2
BSC Young Boys [Switzerland] 2 Fenerbahce [Turkey] 2
AIK Solna [Sweden] 0 Rosenborg BK [Norway] 1
FK Partizan [Serbia] 3 HJK Helsinki [Finland] 0
Ajax Amsterdam [Netherlands] 1 PAOK FC [Greece] 1
Braga Sporting [Portugal] 3 Celtic [Scotland] 0

No comments:

Powered By Blogger