Friday 30 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

David James ahamia Bristol City
Bristol City imefanikiwa kumsaini Kipa Mkongwe David James aliekuwa Portsmouth kwa Mkataba wa Mwaka mmoja huku kukiwa na kipengele cha nyongeza ya Mwaka mmoja.
David James, anaekaribia Miaka 40, ataanza kuichezea Bistola City, iliyo Daraja la Coca Cola Championship, Agosti moja.
James alikuwa pia akitakiwa na Klabu za Celic ya Scotland na Sunderland lakini alishindwa kufikia makubaliano na Klabu hizo.
David James amewahi kuwa Kipa katika Klabu za Liverpool, Aston Villa, West Ham na Manchester City.
Fergie adai zigo kwa Rooney litatuliwa na ‘Chicha’ na Macheda
Sir Alex Ferguson, Bosi wa Manchester United, amedai hana wasiwasi na Javier Hernandez, maarufu kama Chicharito, na Federico Macheda, kwa sababu Wachezaji hao ndio watakaosaidia sana Msimu ujao kumpunguzia mzigo wa kuibeba Timu Wayne Rooney ambao ulimwelemea Msimu uliopita.
Chicharito na Macheda walifunga mabao matamu katika mechi ya Jumatano Man United ilipoinyuka MLS All Stars 5-2 huko Houston, Marekani.
Chicharito alikuwa akicheza Mechi yake ya kwanza kwa Man United.
Ferguson pia alitoboa kuwa wanafikiria kuwatoa Washambuliaji wengine Chipukizi, Danny Welbeck na Mame Biram Diouf, kwa mkopo ili wapate uzoefu.
Ferguson alisema licha ya Chicharito na Macheda kuwa na vipaji pia wana sifa muhimu ya kuwa na nia na ari wakiwa Uwanjani na vitu hivyo ndivyo vimewafanya wawepo Man United.

No comments:

Powered By Blogger