Monday 26 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Man City mbioni kumnasa Supa Mario
Kuna taarifa, ingawa zimepingwa na Wakala, kwamba Mchezaji wa Inter Milan, Mario Balotelli, Miaka 19, yuko mbioni kuungana tena na Roberto Mancini, Kocha ambae ndie aliemwinua na kumwingiza Inter Milan bado akiwa Kinda Mwaka 2006 wakati Mancini akiwa ndie Meneja wa Inter.
Mancini amesema wana nia ya kumchukua Balotelli lakini hawako tayari kulipa dau kubwa kuliko thamani ya Mchezaji huyo.
Tayari Man City imeshawachukua kwa ajili ya Msimu mpya Jerome Boateng, Aleksandar Kolarov, Yaya Toure na David Silva.
Mascherano arudi mazoezini Liverpool
Huku akivumishwa yuko njiani kwenda kujiunga na Meneja wa zamani wa Liverpool, Rafael Benitez, huko Inter Milan, Kiungo Javier Mascherano amerudi Liverpool na kujiunga na wenzake mazoezini kwa ajili ya Msimu mpya ambao kwa Liverpool unaanza mapema mno kwa Mechi ya Mtoano ya EUROPA LIGI ambako Alhamisi Julai 29 watacheza na Rabotnicki ya Macedonia Uwanja wa Anfield na marudio ni Agosti 5 huko Macedonia.
Meneja mpya wa Liverpool, Roy Hodgson, alijaribu kuwasiliana na Mascherano kwa simu alipokuwa likizo lakini hakumpata na mara baada ya Mchezaji huyo kutoka Argentina kutua Liverpool walifanya mazungumzo ili kuwekana sawa kuhusu hali ya baadae.
Hata hivyo haijulikani nini kilifikwa kwenye mazungumzo hayo.
Cudicini arudi kilingeni baada ya ajali mbaya
Kipa wa Tottenham, Carlo Cudicini, ameanza tena kuonekana golini Miezi 8 baada ya kupata ajali mbaya sana ambapo pikipiki aliyokuwa akiendesha kugongwa na Gari na yeye kuvunjika mikono yote miwili pamoja na mfupa wa kwenye kiuno.
Cudicini, Miaka 36, aliidakia Tottenham kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Bournemouth na pia jana walipotoka sare 2-2 na Sporting Lisbon.
Cudicini aliekuwa Chelsea kabla ya kujiunga Tottenham anategemewa kugombea Ukipa Nambari wani hapo Klabuni na Mbrazil Heurelho Gomes ambae ndie Namba moja.

No comments:

Powered By Blogger