Wednesday 28 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Barca imo kwenye lindi la Deni kubwa!!!
Ukaguzi mpya wa Mahesabu wa Mabingwa wa Spain, FC Barcelona, umefichua kuwa Klabu hiyo ipo kwenye Deni kubwa la Pauni Milioni 369.5 na sio Pauni Milioni 11 kama ilivyotangazwa awali na pia Mahesabu hayo yameonyesha Barca imepata hasara ya Pauni Milioni 64 Msimu uliokwisha.
Hivi karibuni, Barcelona ilibidi ikope Pauni Milioni 125 baada ya kushindwa kulipa Mishahara ya Wachezaji ya Mwezi Juni.
Barca wagomewa na Ze Gunners!!!
Msemaji wa Barcelona, Toni Freixa, amesema kuwa mpaka sasa Arsenal hawataki kujadiliana na wao kuhusu kumuuza Cesc Fabregas kwao.
Barcelona walitoa ofa ya Pauni Milioni 29 kumnunua Fabregas Mwezi Juni lakini Arsenal wakaikataa na baada ya hapo kila walipojaribu kuanzisha mazungumzo Arsenal wamegoma kusikiliza chochote.
Freixa ametamka: “Arsenal hawataki kukaa chini na sisi! Tatizo sio sisi au Fabregas, tatizo hawataki kuongea lolote!”
Fabregas bado ana Mkataba wa Miaka mitano na Arsenal ingawa ameshatamka anataka kuichezea Barcelona Klabu ambayo alianzia Soka akiwa mtoto.
Licha ya Klabu yenyewe Barca kujaribu kumrubuni Fabregas, Wachezaji wa Barca ambao Fabregas hucheza nao Timu ya Taifa ya Spain, kina Andres Iniesta, Xavi na David Villa, wamenukuliwa wakimshawishi Fabregas aondoke Ze Gunners na kwenda Barca.
Hata hivyo, licha ya mazungumzo kati ya Barca na Arsenal kukwama hakuna anaejua Barcelona watamudu vipi kumnunua Fabregas hasa ukizingatia hali yao ya kifedha hivi sasa.

No comments:

Powered By Blogger