Saturday 31 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Chicharito aifunga Man United!!!
Katika mechi iliyochezwa Alfajiri ya leo Jumamosi, Julai 31 kwenye ufunguzi wa Uwanja mpya wa Club Deportivo Guadalajara, Klabu ya zamani ya Mchezaji mpya wa Manchester United, Javier Hernandez aka Chicharito, Estadio Omnilife, Mexico, Chicharito alicheza Kipindi cha kwanza akiwa Klabu hiyo ya Mexico na kufunga bao la kwanza dakika ya 8 na Kipindi cha pili akavaa jezi ya Man United na kucheza kwa Robo Saa.
Kila ‘Chicha’ alipopata mpira alikuwa akishangiliwa Uwanja mzima.
Katika mechi hiyo Club Deportivo Guadalajara ilishinda bao 3-2.
Mabao mengine ya Club Deportivo Guadalajara yalifungwa na Bautista dakika ya 38 na Hector Reguoso dakika ya 58.
Mabao ya Man United yalifungwa na Chris Smalling dakika ya 10 na Nani dakika ya 80.
Kikosi cha Man United kilikuwa:
Kuszczak; De Laet (Rafael 65), Smalling, O’Shea, Fabio; Gibson (Nani 46), Scholes (Giggs 65), C.Evans (Fletcher 75), Cleverley; Berbatov (Hernandez 46, Welbeck 65), Diouf (Macheda 65
Wenger: ‘Sheria mpya Wachezaji 25 itavuruga Soka!”
Ingawa Sheria mpya ya kusajili Wachezaji 25 tu na kati yao 8 wawe ‘wamelelewa’ katika Klabu za ama England au Wales kwa Miaka mitatu kabla hawajafikisha umri wa Miaka 21, haiwaathiri sana Arsenal, Meneja wao Arsene Wenger ameiponda kuwa Sheria hiyo itakayoanza kutumika Msimu huu mpya wa 2010/11 kuwa itavuruga Soka.
Licha ya Arsenal kuwa na lundo la Wachezaji ambao ni Wageni, yaani si Raia wa England kama vile Nahodha Cesc Fabregas, Denilson, Gael Clichy, Nicklas Bendtner na Alex Song, lakini hao pamoja na Waingereza Theo Walcott, Jack Wilshere, Aaron Ramsey na Kieran Gibbs, kwenye Sheria hiyo mpya wanafuzu kama Wachezaji ‘waliolelewa’ nyumbani kwa vile walianza kuichezea Arsenal tangu wadogo.
Wenger amedai: “Mie si Shabiki wa Sheria hiyo. Kwanza itawafanya Wachezaji wengi kukosa Klabu! Pili, Klabu zitadhoofika kwenye Soko la Uhamisho wa Wachezaji kwani ukiwa na Wachezaji 25 na ukanunua mmoja unajua sasa una 26 na ni lazima uuze mmoja!”
Wadau wamedai kuwa Wachezaji wengi walio na Miaka 21 na zaidi na ambao hawakuwepo England au Wales kwa Miaka mitatu kabla hawajafikisha umri wa Miaka 21, watajikuta wakipigwa shoka na kukosa Klabu huko England.

No comments:

Powered By Blogger