Friday 30 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Redknapp aponda upangaji Ratiba
Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amelaumu jinsi Ratiba ya Msimu mpya ilivyopangwa na kuwepo kwa mechi za kirafiki kwa Timu za Taifa siku chache kabla Msimu haujaanza.
Tottenham jana ilifungwa na Villareal 4-1 na Jumanne ijayo itacheza na Benfica kisha Fiorentina Agosti 7 zote zikiwa mechi za kujipima nguvu.
Baada ya hapo, Tottenham itawakosa Wachezaji wengi watakaokuwa na Timu za Taifa huku England ikipangiwa kucheza na Hungary Agosti 11.
Tottenham itacheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu England Agosti 14 kwa kupambana na Manchester City na kati ya Agosti 17 na 18 itacheza Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mchujo ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Redknapp alisema: “Huu ni wehu! Tumelundika mechi nyingi! Tunachohitaji ni kufanya mazoezi tu lakini sasa hamna ni mechi baada ya mechi na Wachezaji hupumzika kidogo tu na kucheza mechi nyingine bila mazoezi mazuri!”
Meneja huyo wa Tottenham akaongeza: “Kuna sababu gani kucheza Mechi ya Kimataifa kabla Msimu haujaanza? Hawa walikuwa pamoja Kombe la Dunia na sasa wiki nzima ntawakosa wako Timu ya Taifa na wanarudi Ijumaa na Jumamosi tunacheza na Man City! Hii si sawa!”

No comments:

Powered By Blogger