Tuesday 27 July 2010

CHEKI: www.sokaingongo.com

Campbell kutua Newcastle
Mkongwe Sol Campbell huenda akasaini na Newcastle ikiwa leo atafaulu upimaji wake wa afya baada ya Mkataba wake na Arsenal kumalizika.
Campbell, Miaka 35, alikuwa bado anatakiwa na Arsenal na pia Klabu za Sunderland na Celtic lakini chaguo lake mwenyewe ni Newcastle Timu iliyopanda Daraja Msimu huu baada ya kuporomoka kutoka Ligi Kuu Msimu wa 2008/9.
Ikiwa usajili wa Campbell utakamilika, yeye atakuwa Mchezaji wa tatu kwa Meneja wa Newcastle, Chris Hughton, kusajili kwa ajili ya Msimu mpya, wengine wakiwa ni Dan Gosling kutoka Everton na James Perch toka Nottingham Forest.
Brazil yawaita Rafael na Lucas
Beki wa Manchester United Rafael da Silva nam Kiungo wa Liverpool Lucas Leiva wameitwa kwenye kikosi cha Brazil kitakachocheza Mechi ya kirafiki na USA hapo Agosti 10.
Kikosi hicho cha Brazil ndio uteuzi wa kwanza wa Meneja mpya wa Brazil, Mano Menezes, na Rafael na Lucas ni Wachezaji pekee kutoka Ligi Kuu England.
Menezes amewachukua Wachezaji wanne tu toka Kikosi cha Brazil kilichocheza Kombe la Dunia huko Afrika Kusini ambao ni Dani Alves, Ramires, Thiago Silva na Robinho.
Hii ni mara ya kwanza kwa Rafael kuitwa kuichezea Brazil lakini Lucas itakuwa mara yake ya tatu.
Wachezaji 11 kati ya 24 waliotajwa na Menezes kwa ajili ya Mechi hiyo na USA itakayochezwa New Jersey, Marekani, ni wapya kwa Brazil.
Kikosi kamili ni:
Makipa: Jefferson (Botafogo), Renan (Avai), Victor (Gremio) Mabeki: Andre Santos (Fenerbahce), Dani Alves (Barcelona), Marcelo (Real Madrid), Rafael da Silva (Manchester United), David Luis (Benfica), Henrique (Racing Santander), Rever (Atletico Mineiro), Thiago Silva (AC Milan)
Viungo: Carlos Eduardo (Hoffenheim), Ederson (Lyon), Paulo Henrique Ganso (Santos), Hernanes (Sao Paulo), Jucilei (Corinthians), Lucas Leiva (Liverpool), Ramires (Benfica), Sandro (Internacional)
Mafowadi: Alexandre Pato (AC Milan), Andre (Santos), Diego Tardelli (Atletico Mineiro), Neymar (Santos), Robinho (Santos, on loan from Manchester City)
Hodgson: “Mascherano anataka kuhama Liverpool!”
Meneja wa Liverpool, Roy Hodgson, amethibitisha kuwa Javier Mascherano anataka kuhama lakini amethibitisha Fernando Torres atabaki.
Mascherano, Miaka 26, amehusishwa sana na kuhamia Inter Milan ili kuungana tena na aliekuwa Meneja wa Liverpool, Rafael Benitez, ambae ndie Kocha mpya wa Klabu hiyo ya Italia.
Hodgson amesema: “Ndio anataka kuondoka. Alitaka kuhama tangu Msimu uliokwisha. Lakini bado ana Mkataba na Liverpool hivyo uamuzi wa kuhama ni wetu na si yeye.”
Kuhusu Torres, Hodgson amesema bado yuko likizo na atajiunga na Liverpool Jumatatu ijayo lakini atabakia hapo kwa vile bado anaifurahia Anfield.

No comments:

Powered By Blogger