Wednesday 28 July 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Liverpool kuanza EUROPA LIGI bila Mastaa
Roy Hodgson ameruka na Kikosi chake cha Liverpool kwenda Macedonia kupambana na FK Rabotnicki kwenye mechi ya kwanza ya Raundi ya 3 ya Mtoano wa EUROPA LIGI hapo kesho bila Mastaa wake wakubwa kama Nahodha Steven Gerrard, Jamie Carragher na Mchezaji mpya Joe Cole ambao wote walikuwa Timu ya England kwenye Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na ambao ndio kwanza wamerudi mazoezini baada ya kupewa muda zaidi kupumzika.
Kikosi cha Liverpool cha Wachezaji 20 kilichosafiri kina Chipukizi kina Jonjo Shelvey, Nathan Eccleston, Martin Hansen, Peter Gulacsi, David Amoo, Lauri Dalla Valle na Tom Ince.
Wachezaji wazoefu waliokuwemo ni Martin Skrtel, Daniel Agger, Sotirios Kyrgiakos, pamoja na Wachezaji wapya Milan Jovanovic na Danny Wilson.
Kikosi kamili ni: Cavalieri, Aquilani, Agger, Jovanovic, Kyrgiakos, Lucas, Wilson, Ngog, Spearing, Darby, Shelvey, Kelly, Skrtel, Eccleston, Ayala, Hansen, Gulacsi, Amoo, Dalla Valle, Ince
Drogba si biashara!
Mkurugenzi Mkuu wa Chelsea, Ron Gourlay, ameufuta uvumi kuwa Didier Drogba anahama Stamford Bridge kufuatia kauli ya Wakala wake, Thierno Seydi, kudai Drogba huenda akatua Manchester City.
Gourlay amesema Drogba, mwenye Miaka 32 na mwenye Mkataba na Chelsea hadi 2012, atabakia hapo Msimu huu na kwamba wao wamezoea wakati kama huu kila Msimu kusikia kuhama kwa Mastaa wao.
Bosi huyo wa Chelsea, ambayo tayari imechukua Wachezaji wapya wawili, Yossi Benayoun toka Liverpool na Tomas Kalas, amesema Meneja wao Carlo Ancelotti yuko huru kuongeza Wachezaji akihitaji.
Raul atua Bendsliga na Schalke 04
Mkongwe na Staa wa Real Madrid ambae ameondoka Klabu hiyo ya Spain amesaini Mkataba wa Miaka miwili na Klabu ya Ujerumani Schalke 04.
Raul alidumu Real kwa Miaka 18 na kuchezea mechi 741 na kufunga magoli 323.

No comments:

Powered By Blogger